Changamoto Zinazokumba Shirika la Utangazaji la Uganda Katika Kukikuza Kiswahili Jijini Kampala

Abstract

Kiswahili nchini Uganda kimetumiwa tangu enzi za kabla ya ukoloni katika tasnia mbalimbali ila bado hakijaenea kama inavyostahili. Licha ya kuwa Uganda kuna sera, mazoea, na utaratibu wa kuendeleza Kiswahili, bado kina wakati mgumu kupenyeza kila mahali huku baadhi ya jamii ya Wanauganda wakibaki kuwa na mtazamo hasi kuhusu lugha hii adimu. Tafiti za awali zilionyesha kuwa mashirika ya utangazaji ya serikali ni muhimu sana katika kukuza lugha za mawasiliano ulimwenguni. Nchini Uganda, mtafiti hajakumbana na utafiti unaoonyesha chanagamoto zinazolikumba Shirika la Utangazaji la Uganda katika kukuza lugha ya Kiswahili. Kwa hivyo utafiti huu ulinuia kutathmini changamoto zinazokumba Shirika la Utangazaji la Uganda katika kukikuza Kiswahili jijini Kampala. Utafiti ulitumia nadharia ya upangaji lugha kubaini hasa jinsi shirika hilo lenye vituo kumi na moja vya redio na vinne vya televisheni linavyokumbana na changamoto za kukuza Kiswahili katika jiji kuu la Kampala. Kwa kutumia nadharia hiyo utafiti uliegemea sana itikadi nne za upangaji lugha na vipengele vinne vya mchakato wa usanifishaji wa lugha hasa kile cha uimarishaji wa lugha. Mbinu za kurekodi, mahojiano, uchunzaji wa kushiriki na kusoma maktabani zilitumika katika kukusanya data. Sampuli ya utafiti huu kwa jumla ilihusisha watu 30 wakiwemo watumishi 20 wa Shirika la Utangazaji la Uganda ambapo 10 ni Waandishi Habari za Kiswahili. Watu 10 waliosalia waliteuliwa kutoka hadhira ya Shirika la Utangazaji la Uganda jijini Kampala. Utafiti huu uliwalenga wasikilizaji, watazamaji, watumishi wa makao makuu ya Shirika la Utangazaji Uganda jijini Kampala kwa vile wao ndio wadau waliochangia kwa kufanikisha madhumuni ya utafiti huu. Utafiti huu ulibainisha kuwa kuna wataalamu wachache katika lugha ya Kiswahili, ukosefu wa wahisani na ufadhili, kutokuwepo kwa sera madhubuti ya uhariri kuhusu Kiswahili, uhaba wa vitendea kazi na mitazamo hasi kwa lugha ya Kiswahili ni baadhi ya changamoto zinazokumba shirika la Utangazaji la Uganda katika harakati zake za kuendeleza lugha ya Kiswahili. Utafiti huu una manufaa kwa wizara zinazoshughulika na maendeleo ya Kiswahili Uganda kwa sababu vile utawapa mwanga kuhusu changamoto zinazolikumba Shirika la Utangazaji la Uganda katika harakati za kukukuza Kiswahili.

Description

Keywords

Changamoto, Shirika la Utangazaji, Kukikuza Kiswahili, Kampala.

Citation

Collections

Endorsement

Review

Supplemented By

Referenced By