Udhalilishaji wa Asasi Kuu za Kijamii katika Muziki wa Kisasa
No Thumbnail Available
Date
2024-08-20
Authors
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
Laikipia University
Abstract
Muziki wa Kisasa ni mojawapo wa muziki maarufu sana kwa vijana nchini Kenya. Licha ya
kuwa kitumbuizo kwa vijana, muziki huu hutumika kama nyenzo ya kuwazindua vijana ambao
wako kwenye shinikizo zito kutokana na matatizo yanayowakumba katika jamii. Tangu miaka
na mikaka, binadamu amekuwa akitoa hisia zake: za uchungu, kero, mafadhaiko au furaha
kupitia muziki ambao husawiri mazingira yake. Mintarafu ya hayo, makala haya yalichunguza
jinsi muziki wa kisasa unatumika kudhalalisha asasi kuu za kijamii ambazo badala ya kutoa
suluhisho la matatitzo chungu nzima yanayowakumba vijana, asasi hizi ndizo chanzo kuu cha
matatatizo hayo. Mawazo ya Jean-Francois Lyotard katika nadharia ya usasaleo kuhusu
udhalilishaji wa tamaduni na asasi kuu zinazokandamiza maisha ya watu kwani haziakisi hali
halisi ya maisha yalikuwa dira katika uchunguzi huu. Muundo wa utafiti huu ulikuwa wa
kiuthamano na kimaelezo na ulifanyika maktabani. Data ya msingi katika utafiti huu ilikuwa
nyimbo tano za Genge ambazo zilipakuliwa mtandaoni. Makala haya yanaonyesha kwamba
Muziki wa Kisasa umewapa vijana jukwaa la kudhalilisha asasi kuu kama vile dini, lugha na
vyombo vya dola kwani vinawasababishia vijana mahangaiko mengi. Udhalilishaji wa asasi kuu
katika tungo zao umewapa vijana njia salama ya kujikomboa kutokana na mifumo ya awali
ambayo haikuwapa nafasi ya kujieleza wala kuruhusu mabadiliko. Matokeo ya utafiti huu yatakuwa malighafi katika taaluma za isimu na fasihi pamoja na uchanganuzi diskosi matini
Aidha matokeo ya utafiti huu yatotoa mwanga kuhusu maswala yanayowakumba vijana hivyo
basi ni marejeleo muhimu kwa washika dau wote wanaobuni sera na mikakati kabambe ya
kuwainua vijana ambao ni nguzo muhimu katika jamii.
Description
Keywords
Asasi kuu, muziki wa kisasa, udhalilishaji, usasaleo, vijana