Mercy Muthoni Kariuki1*, Prof. James Onyango Ogola, PhD1 na Prof. Nabea Wendo, PhD12026-02-102025-01-252707-3475https://doi.org/10.37284/2707-3475http://41.89.103.50:4000/handle/123456789/1385Utabaka ni hali ya kuwagawanya watu kwa misingi ya uwezo wao wa kumiliki wa mali ilhali ukengeushi ni hali ya kumfanya mtu afuate njia ambayo si nzuri kwa kumlaghai. Hali hii husababisha migogoro miongoni mwa wahusika. Tamthilia ni kipengele cha fasihi andishi kinachowasilisha ujumbe kwa kutumia mazungumzo baina ya wahusika. Tafiti za awali katika tamthilia zilishughulikia matumizi ya lugha, mandhari, na uhusika katika tamthilia. Katika kupitia tafiti na makala mengine ya awali, mwandishi hajakumbana na tafiti kuhusu masuala ya utabaka na ukengeushi katika tamthilia ya Kigogo. Hili ndilo pengo la kiusomi ambalo lilichochea utafiti huu kufanywa ili kulijaza. Makala yalinuia kutathmini athari za utabaka na ukengeushi katika tamthilia ya Kigogo iliyoandikwa na Pauline Key. Matini yalichanganuliwa kwa kutumia misingi ya nadharia ya umarx iliyoasisiwa na Karl Heinrich Marx na kuendelezwa na wataalam kama Karl Kautsky, George Plekhanov na György Lukács. Utafiti ulifanywa maktabani ambapo athari za utabaka na ukengeushi kutokana na usomaji wa kina yalidondolewa kwa minajili ya uchanganuzi na uwasilishaji kwa kutumia mihimili ya nadharia ya umarks. Tamthilia hii ilichaguliwa kimaksudi kwa sababu inaangazia athari za utabaka na ukengeushi ambayo ndiyo mada ya makala haya. Mbinu ya kimaelezo ilitumiwa katika kuwasilisha na kuchanganua data. Usomaji wa kina wa tamthilia hii ulibainisha kuwa utabaka na ukengeushi husababisha ufisadi, ukosefu wa kazi, uchafuzi wa mazingira, ukosefu wa maendeleo, mapendeleo, kufungwa kwa soko, mauji, usherati, unyakuzi wa mashamba, chuki, uvamizi na ukombozi. Makala haya yana mchango katika uchambuzi wa vitabu teule vya fasihi andishi katika kueleza maudhui ya utabaka na ukengeushi. Utafiti huu pia ulitumiwa kama mwongozo kwa wasomi wengine watakaofanya utafiti katika fasihi andishi.enUtabakaUkengeushi na TamthiliaTathmini ya Athari ya Utabaka na Ukengeushi Katika Tamthilia ya KigogoArticle